Sponsor

banner image

recent posts

Sitasahau: Tulitolewa nduki ukweni siku ya posa




Nilikuaga na mpenzi wangu tunapendana kwa kweli toka chuoni (UDSM) basi tukawa tunapiga mechi peku peku (bila kondom) eeh ghafla bidada ananiambia ana mimba kiukweli nilishtuka but anyway tukakubaliana azae tu.

Basi bibie akaja kujifungua mtoto (mimi sikujitokeza huko ukweni kabisaa)mi nawasiliana na mchuchu tu. 

Sasa tukakubaliana na mchuchu ni muda muafaka wa kwenda kujitambulisha. 

Nikaandaa mshenga na ndugu wa karibu kwenda huko. Duuh ile kufika tu tukamkuta baba mzaa chema kakunja sura balaa ile tunapiga hodi anatuangalia tu (hajibu chochote) ghafla akaingia chumbani akatoka na panga.

Hakuna aliyeaga si mshenga wala mimi. "BA MKWE" anadai nilimzalisha mtoto wake na sijajitokeza siku zote.

Jamani sitamsahau yule mzee.
Sitasahau: Tulitolewa nduki ukweni siku ya posa Sitasahau: Tulitolewa nduki ukweni siku ya posa Reviewed by Love Psychologist on March 13, 2019 Rating: 5

No comments:

Powered by Blogger.