Sponsor

banner image

recent posts

Uzi maalum wa kuzidi kuwapa morali wasiochepuka na hasara zakuchepuka



Wakuu habari za muda.
Kama kichwa cha habari kinavosema hapo juu,wanaochepuka wanaanzisha nyuzi zao mbali mbali kusifia mambo yao hayo huku wakiwatamanisha wasiochepuka waanze mchezo huo.

Sasa leo na sisitusiochepuka au wenye mpango wa kuacha tuanzishe wetu hapa kuelezana hasara zake na vile mtu unajiskia baaa ya kuchepuka,na vile ambavyo kuchepuka hakuna ishu.
Mimi naanza.

Kuchepuka ni kujidanganya tu kwa sababu unatafuta kitu kimoja kutoka kwa wanawake weeeeengi.ilhali mkeo anacho ni suala la kukaa kuzungumza tu.

Wakati huo mwanamke anahitaji vitu viiiingi kutoka kwa mwanaume mmoja ambae ni mumewe.hivyo wanawake ndo walikuwa na chansi kubwa ya kuchepuka kwa sababu wanahitaji vingi ili nyoyo zitulie lakini wengi wao waaminifu sana hawachepuki.lakini we mwanaume unahitaji ngono tu wanawake teleee.umeona ulivyokuwa huwezi kustahamili anakushina hadi demu anayehitajia mahitaji mengi?

Hakuna anayechepuka kutafuta tabia nzuri aisee,sasa ikiwa mkeo anatabia safi unadhani tatizo lake ukimuambia hatolielewa?
Au kama ana kasoro ya maisha unadhani ni sahihi kumchepukia kwa kasoro yake Mkuu?
Kama ni sahihi jaribu kujiuliza tu kwa nini ulimuoa?
Kama kaipatia kwenye ndoa(kasoro) basi rudisha fikra upande wa pili jeee wewe ungependa ufanyiwe hivyo?

Alafu kuchepuka bhana ujinga wake sasa : utamfatilia deeemu ukamuona wa maana sana,ukila siku mbili tu unamchoka unaanza kukodolea macho wengine hali yako inakuwa hiyo hiyo,unajua kwa nini?

Hivi ikiwa hutosheki na chakupika na kujipakulia mwenyewe utaweza kutosheka na vya kuonjeshwa? (nadhani muumeelewa)

Sasa ishu ni kuridhika na yule uliyemtolea mahari tu,nyuchi zote ziko vile vile,hata iwe nzuri vipi,hata ibane vipi kama awamu ya tano lakini bado utaiwacha tu na hufikirii mwisho wake ni mzuri au mbaya?

Alafu pia mchepuko unakufanya uzidi kuchepuka zaidi,unajua kwa nini?

Si unajua kwamba unapotafuta mchepuko una lengo la kutegemea mazuri enh na ndiyo mana ukamsaliti mkeo?
Sasa huyo mchepuko utaiona kasoro tu ambayo utashawishika utafute mwingine na utaishi hivyo hivyo maisha yako yote,ushafikiria mwisho wake nini?

Kufa kwa maradhi?

Au kuacha huo mchezo?

Au kufedheheka?

Changamoto zipo lakini ndiyo zinazotuamulia vipi tuwe kwa namna tunavozipokea changsmoto.
Mfano :changamoto ya mke akiwa katika siku zake mume huli menyu,hii changamoto unatakiwa uikabili lakini ukiishindwa jua tu kwamba unataka kushindana na uhalisia,utatafuta mchepuko lakini je nao haueni hedhi? Kama unaenda si bora ungebaki na mama john tu maisha yaendelee?
Na huo mchepuko utatamani kuzaa n.k huko utatafuta ungine(watotoz)na umri wako kumbuka unaenda.utaishi hivyo hivyo.


Endelezeeni wadau kupinga michepuko.....
Uzi maalum wa kuzidi kuwapa morali wasiochepuka na hasara zakuchepuka Uzi maalum wa kuzidi kuwapa morali wasiochepuka na hasara zakuchepuka Reviewed by Love Psychologist on May 04, 2019 Rating: 5

No comments:

Powered by Blogger.